Sunday, November 29, 2009

Mtagwa kurejea ulingoni Jan 23 kuwania mkanda wa WBA.

Image courtesy of http://www.phillyboxinghistory.com/
Baada ya kupoteza pambano lake kiutatanishi Oktoba 10 dhidi ya Juan Lopez na kukataliwa pambano la marejeano licha ya kuonesha uwezekano mkubwa wa "kumuumbua" Lopez, bondia mTanzania aishiye Philadelphia Rogers "The Tiger" Mtagwa atapanda ulingoni Jan 23, 2010 kupambana na bondia anayefanya vema saana na nyota ing'aayo toka Cuba Yuriorkis Gamboa.
Pambano hilo litakalopiganiwa New York na kuonekana kupitia HBO, litakuwa ni la kuwania mkanda wa Gamboa wa uzito wa Unyoya (featherweight) unaotambuliwa na Chama cha Ndondi Ulimwenguni (WBA). Usiku huohuo na katika ukumbi huohuo, Juan Manuel Lopez ambaye alipata ushindi dhidi ya Mtagwa atapambana na Steven Luevano kuwania mkanda wa Shirikisho la Ndondi Ulimwenguni (WBO) unaoshikiliwa na Luevano.
Iwapo Mtagwa atavuka kigingi hiki kigumu (kulingana na ubora na upiganaji wa Bwana mdogo Gamboa) atakuwa amejiweka katika mazingira mazuri ya kurejea ulingoni na Lopez kama wataweza kuafkiana katika kuunganisha mikanda kwani yote ni ya uzito mmoja.
Hapa chini ni Video ya pambano la Mtagwa la mwezi uliopita

Kila la kheri katika maandalizi yako Kaka Mtagwa.

Saturday, November 28, 2009

EID MUBARAK

Friday, November 27, 2009

Tanzania Yangu.....Iliyo "bize" kumwagilia matawi badala ya mizizi


NAJUA LEO NI IJUMAA NA NILISTAHILI KUBANDIKA TOKA LABEL YA I & THEM LAKINI NAOMBA NIIZUNGUMZIE TANZANIA YANGU
Katika beti ya kwanza ya wimbo wake GUNS & ROSES, Lucky Dube aliimba "I don' t know why I keep believing that one day they' ll bring us together. When they' ve shown in more ways than one that all they care about is the dollar"
Ndilo ninalowaza sasa kuhusu WANASIASA wa nchini mwangu Tanzania ambao wanaonekana kutojiandaa kwa lolote jema wanalotaka kufanya.
Bwawa la uzalishaji umeme la Kidatu Image from http://www.industcards.com/hydro-africa.htm. Bwawa la uzalishaji umeme la Kihansi Image from http://www.industcards.com/hydro-africa.htm.
Nimemsikia Rais Kikwete bila aibu akiwaalika wawekezaji huko Jamaica wakati waTanzania wana mgao wa umeme unaozidi nusu ya siku yao.

Angalia uwiano wa ubora baiskeli na mavazi na viatu. Na bado twategemea kwenda Olimpiki. Image from http://www.issamichuzi.blogspot.com/
Rais wangu huyohuyo anazungumzia mafanikio ya michezo ya Jamaica na kuyataka Tanzania ilhali wamefuta michezo mashuleni na hata iliyopo haina viwango wala usawa

Taswira za Polisi Msimbazi... Yaani Dar Es Salaam katikati ya jiji. Sijui mikoani kukoje
Kweli mtu aishi kwenye magofu haya na bado aipende kazi wakati "mafisadi" wanaishi kama wako nusu peponi?? Picha toka http://mtwarakumekucha.blogspot.com/
Ninasikia wakisema kutokomeza uhalifu na kutaka askari kuwa waadilifu ilhali maisha ya nyumbani kwao yako hivi.

Ndiyo mazingira yatuzungukayo hayo na kuna Halmashauri zinazotukata kodi. Askari wa jiji wanaokimbiza na kupora Mama ntilie na Machinga wasisimamie usafi. Picha toka http://mtwarakumekucha.blogspot.com/

Twawasikia wakizungumzia AFYA YA MLAJI na kuzungumzia kuboresha afya ya mtanzania na urefu wa maisha yake. Lakini utekelezaji ndio huo tuuonao. Yaaniiii.............

Hawa ndio viongozi wetu wa kesho. Lord Have Mercy. Picha toka Michuzi Jr blog na Mch. Emmanuel Bwatta kupitia Adam L. wa blogu ya http://www.upole.blogspot.com/

Na mwisho twasikia mpango wa Kompyuta kwa wote japo twajua hata ubao wa kuandikia una utata. Hakuna ukuta na hata ezekeo ni la ajabu. Hakuna viti wala madawati na nina wasiwasi kama waalimu ofisi zao si nyumbani mwao.
Ninachojiuliza hapa ni kwanini Rais na viongozi wengine waanze kushughulikia kuhusu UWEKEZAJI wakati hata Barabara, Maegesho na mitaro ya maji taka haijajengwa? Kuleta wawekezaji ilhali wasomi hawapo nyumbani ni sawa na kuwaambia wawekezaji kuwa WATATAWALA MILELE kwani hakuna atakayekuja kuchukua nafasi yao.
Kwanini tusiboreshe Makazi ya Askari, Kwanini tusihakikishe wanafunzi wote wanasoma katika mazingira yanayowapa muda wa kufikiria masomo na mazingira ya masomo?
Wamekaa wakiwekeza kwenye kumwagilia matawi huko kwenye vikao waendako ilhali mizizi ya hapa nyumbani inakauka.
HAWATAFANIKIWA KAMWE kwani wanamwagilia kisicho sahihi.
Tanzania Yangu ni kipengele kinachozungumzia ytale yaendeleayo nchini Tanzania na namna ambavyo "ndivyo sivyo" inavyozidi kupamba moto nchini. Kwa matoleo yaliyotangulia BOFYA HAPA
Tuonane "Next Ijayo"

Thursday, November 26, 2009

Nalinganisha majengo na uchumi wetu

Nawaza kwa sauti tu. Kulingana na uchumi na uhitaji wa wahitaji wa nchi hizi, ni nchi ipi ilistahili kuwa na jengo lipi la bunge la nchi yake?
Bunge la Uingereza
Bunge la Tanzania

Kutoka Bloguni!!!! Twende majaridani na magazetini

Kakangu Albert wa blogu ya MWANGAZA aliwahi kuuliza kuhusu itakavyokuwa kama makala nono ziandikwazo kwenye blogu zetu zingeweza kufika kwenye magazeti. Tukawa tunawafikia kina Bibi yangu kule Bushasha na wengine mikoani. Lakini si jambo geni kwani tuliwahi kulijadili siku ileeeee ambayo Da Koero aliandika kuhusu Yasinta. Na binafsi nikachukua hatua moja mbele na kumwambikia mhusika wa Gazeti tuliloona lina nafasi kubwa ya kutuunga mkono kwani ni la mwana-blog na lina wana-blog wengi la KWANZA JAMII kuhusu hili.
Na leo nilipofungua hapa kwa Da Koero na kukuta anahamasika kusogea gazetini nikajumiisha na maandishi haya ya Kaka Matondo nikaona ni vema kukumbushana kuwa kutakuwa na manufaa na itawafaa JAMII ambayo tunahangaika kuielimisha na kuikomboa.
Barua yangu kwa KWANZA JAMII ilisema


Kutoka bloguni
Saturday, April 18, 2009 3:24 PM
From:
"Mubelwa T. Bandio"
View contact details
To:
habari@kwanzajamii.com
Amani, Heshima na Upendo kwenu nyote.
Natumai kuwa mu-wazima na mnaendelea vema na harakati za kuikomboa jamii. Kwanza niwapongeze kwa ujio wa gazeti jipya lenye uelimishaji. Gazeti lenye mchanganyiko wa chambuzi na kuonekana kuwa na mtazamo wa kuinusuru jamii.
Pia katika nililogundua ni kuwa gazeti hili lina timu ambayo wengi wao pia ni waandishi wa blogu mbalimbali za ki-chambuzi. Kwangu ni nyota njema kuwa waandishi wa blogu wana nafasi nzuri ya kuweza kusogeza habari kutoka kwenye mfumo huu kwenda kwenye uchapishaji (japo wengine ndiko walikoanzia). Lakini nakumbuka kuwa wiki chache zilizopita mmoja wa wana-blog (Dada Koero Mkundi wa www.koeromkundi.blogspot.com ) aliandika habari kumhusu binyi mmoja aitwaye Yasinta ( http://koeromkundi.blogspot.com/2009/03/kutana-na-yasinta-mjasiriamali.html) ambayo iliwagusa wasomaji wengi na kukawepo na maoni ya namna ya kuwezesha kufikisha habari kama hizo "nje ya blogs" na kuna waliosema wangekunadikia kuomba ufikirie hili. Sina haika kama walifanya hivyo, bali nami nimeona niandike kuona kama unaweza kufikiria kuwa na "kona" ya kutoka bloguni ambayo kwa kutumia waandishi wa blog wanaoandika kwenye Kwanza jamii mkaweza kuchagua habari kutoka blog mbalimbali mnazohisi zinaifaa jamii yetu.
Ni hayo tu na naamini utayafikiria.
Blessings

Wednesday, November 25, 2009

Labda "akutendeaye mabaya" ndiye akujaliye!!!!

Mara kadhaa katika blogu zetu za kimaandishi tumejadili kuhusu suala la UBAYA. Kuanzia kuuangalia kama upo mpaka kuona kama kile kiitwacho ubaya kama kina faida na kisha kuangalia kama tunahusisha lile liitwalo UBAYA na matukio halisi ya maisha yetu. Tumejadili pia kuhusu KUWAOMBEA WALE TUWAONAO KAMA ADUI ZETU kwa kuwa nao wana nafasi kuuubwa saana katika ukuaji wetu. Yaani wanapojitahidi kuhakikisha tunashindwa, wanatuongezea moyo na maarifa ya kufanya vema zaidi. Watu hawa pia ni muhimu saana kwetu. Lakini pengine la kujiuliza ni kuwa LIPI TUONALO KAMA UBAYA?? Unadhani tafsiri yako ya UBAYA inaweza kuwa na ukweli katika kuleta suluhisho la nani kakufanyia nini? Waswahili wanasema TENDA WEMA NENDA ZAKO, nami najiuliza kama ukitenda wema (ilhali atendewaye auona kama ubaya) kisha ukaenda zako unadhani mtendewa atagundua kuwa ni wema kama halitatokea baya zaidi ya ulilomtendea??
Ninavyozidi kuishi nazidi kugundua kuwa pengine akuibiaye sasa hivi shilingi laki moja anakukumbusha na kukuonya kuwa mahala hapo si salama na usiwe unabeba pesa hovyo kabla hujajenga tabia hiyo na kuanza kutembea na milioni kisha zikaibiwa.
Labda mkioana na kuachana ndani ya miezi michache si mkosi bali yaweza kuwa nafuu kuliko kusubiri baada ya miaka kumi ya kuchuma pamoja na watoto kadhaa kisha mmoja wenu analazimika kubaki kwa ajili ya "matunda" hayo mlovuna pamoja.
NI WAKATI AMBAO TUNATAKIWA KUTUMIA KILA KITUKUTACHO KUJIFUNZA NA SI KULAUMU NA KULALAMA
Labda nikukumbushe "hadithi" hii inayoweza kuoanisha vema nisemayo na "kichwa cha habari"

IF YOU ARE UNHAPPY.
Once upon a time, there was a noncomforming sparrow who decided not to fly south for the winter. However, soon the weather turned so cold that he reluctantly started to fly south. In a short tile ice began to form on his wings and he fell to earth in a barnyard, almost frozen. A cow passed by and crapped on a little sparrow. The sparrow thought it was the end. But, the manure warmed him and defrosted his wings. Warm and happy, able to breathe, he started to sing. Just then a large cat came by and hearing the chirping, investigated the sounds.
The cat cleared away the manure, found the chirping bird and promptly ate him.

THE MORAL OF THE STORY
1: Everyone who shits on you is not necessarily your enemy.
2: Everyone who gets you out of the shit is not necessarily your friend.
And
3: If you're warm and happy in a pile of shit, keep your mouth shut.

Tuesday, November 24, 2009

Hongera wana-STRICTLY GOSPEL

Kwa muda sasa tumekuwa tukijaribu kupiga hatua ya ziada kwenye uhabarishaji na uelimishaji wetu kuwagusa wengi wahitajio lakini hawana namna ya kupata habari ihizi kupitia mtandao. Tumejadili kuhusu kuweka makala na maandishi yetu kwenye MAGAZETI na MAJARIDA na bado naamini tutafanikisha jambo hili ili tuweze kuwafikia wengi zaidi.
Kwa sasa niwapongeze wanaSTRICTLY GOSPEL kwa kufanikiwa kuvuka kizingiti hiki kwa kuweza kuanza kuchapisha jarida lao liendalo kwa jina hilohilo.

Wamesonga hatua moja mbele kutoka wana-mtandao pekee (blog) mpaka mtandao na jarida.
JIANDAE KUPATA NAKALA YA JARIDA HILI HIVI KARIBUNI

Monday, November 23, 2009

Za Kale vs Maisha ya Sasa..........MWISHO WA MWEZI

Na hizi ndizo tarehe. Tarehe za UNDUGU KUKUA, tarehe za wengine kuzikimbia nyumba zao (halisi), tarehe za wengine kuvesha vimada, tarehe za kinamama wauza "pampula (pombe za kienyeji) kuona ongezeko la mapato, tarehe za watu kuzhelewa kurejea nyumbani, tarehe za nyimbo kuongezeka uziku toka kwa walevi wanaotoka vilabuni, tarehe za vipigo kuongezeka ndani ya nyumba (kwa kuwa tu fulani kauliza amechelewa wapi), tarehe za wezi kujiajiri zaidi (kwani wanajua mifuko imetuna), tarehe za wengine kuhatarisha maisha ya wengine.
Hivi nimesema kuhusu tarehe za wengi kuambukizwa maradhi (kwa kuwa tu wamelewa na kila aliye mbele yao ni mrembo hata kama kaathirika). Ndio zileee siku ambazo Prof Jay alisema ni "mwendo wa viti virefu jirani na nyama choma na toto mbili tatu ..........hii watu wa pombe wanasema ni kupoteza mawazo ingawa mara nyingi hutokea wakati unazo"
Ni mwisho wa mwezi. Wenye mambo na vijambo. Ambao kila ufikapo basi wengi twajua iwavyo. Ni "mishemishe" kila mahala, kila mtu ni "busy" kwa kwenda mbele na kwa hakika muda unaohitaji umakini kwani watu wanakuwa wanaendeshwa na pesa kuliko akili zao binafsi.

MWISHO WA MWEZI una mambo mengi na kama unashani yalianza sasa hivi, sikiliza Vijana Jazz Band (enzi za kina Hayati Hemedi Maneti na Eddie Sheggy) wanavyokukumbusha tangu enzi hizo jinsi mwisho wa mwezi ulivyokuwa.
** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia siku za Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mitandao shirika hapa**