Mara kadhaa katika blogu zetu za kimaandishi tumejadili kuhusu suala la UBAYA. Kuanzia kuuangalia kama upo mpaka kuona kama kile kiitwacho ubaya kama kina faida na kisha kuangalia kama tunahusisha lile liitwalo UBAYA na matukio halisi ya maisha yetu. Tumejadili pia kuhusu KUWAOMBEA WALE TUWAONAO KAMA ADUI ZETU kwa kuwa nao wana nafasi kuuubwa saana katika ukuaji wetu. Yaani wanapojitahidi kuhakikisha tunashindwa, wanatuongezea moyo na maarifa ya kufanya vema zaidi. Watu hawa pia ni muhimu saana kwetu. Lakini pengine la kujiuliza ni kuwa LIPI TUONALO KAMA UBAYA?? Unadhani tafsiri yako ya UBAYA inaweza kuwa na ukweli katika kuleta suluhisho la nani kakufanyia nini? Waswahili wanasema TENDA WEMA NENDA ZAKO, nami najiuliza kama ukitenda wema (ilhali atendewaye auona kama ubaya) kisha ukaenda zako unadhani mtendewa atagundua kuwa ni wema kama halitatokea baya zaidi ya ulilomtendea??
Ninavyozidi kuishi nazidi kugundua kuwa pengine akuibiaye sasa hivi shilingi laki moja anakukumbusha na kukuonya kuwa mahala hapo si salama na usiwe unabeba pesa hovyo kabla hujajenga tabia hiyo na kuanza kutembea na milioni kisha zikaibiwa.
Labda mkioana na kuachana ndani ya miezi michache si mkosi bali yaweza kuwa nafuu kuliko kusubiri baada ya miaka kumi ya kuchuma pamoja na watoto kadhaa kisha mmoja wenu analazimika kubaki kwa ajili ya "matunda" hayo mlovuna pamoja.
NI WAKATI AMBAO TUNATAKIWA KUTUMIA KILA KITUKUTACHO KUJIFUNZA NA SI KULAUMU NA KULALAMALabda nikukumbushe "hadithi" hii inayoweza kuoanisha vema nisemayo na "kichwa cha habari"
IF YOU ARE UNHAPPY.
Once upon a time, there was a noncomforming sparrow who decided not to fly south for the winter. However, soon the weather turned so cold that he reluctantly started to fly south. In a short tile ice began to form on his wings and he fell to earth in a barnyard, almost frozen. A cow passed by and crapped on a little sparrow. The sparrow thought it was the end. But, the manure warmed him and defrosted his wings. Warm and happy, able to breathe, he started to sing. Just then a large cat came by and hearing the chirping, investigated the sounds.
The cat cleared away the manure, found the chirping bird and promptly ate him.
THE MORAL OF THE STORY
1: Everyone who shits on you is not necessarily your enemy.
2: Everyone who gets you out of the shit is not necessarily your friend.
And
3: If you're warm and happy in a pile of shit, keep your mouth shut.