Thursday, September 7, 2023

Darasa 45: Maisha yetu kama zoezi la matofali


Darasa linakukumbusha kuwa...… Watu watatu ni mimi na wewe. Watu kumi ni mimi na wewekwa sababu kuna watu tumesimama nyuma yao. Lakini pia, ni watu wetu wa karibu wanaosimama nyuma yetu. Mtu wa kwanza ni yule ambaye anapokuwa na kitu cha kutimiza hasubiri watu wakimbie pamoja naye. Huchakarika kadiri ya uwezo wake bila kulalamika wala kuvunjika moyo kwa kuwa hana msaada. Mtu wa pili ni yule ambaye anapokuwa na jambo lake ni lazima apate msaada ndiyo alifanye kwa kasi. Mtu wa hivi bila kusukumwa haendi wala hawajibiki ipasavyo. Ni ngumu kutimiza mambo yake ipasavyo bila kuegemea wengine. Mtu wa mwisho ni yule ambaye ni mlalamishi. Hutaka jambo lake watu wote waache shughuli zao kwa ajili yake. Hata kwenye ambayo ni wajibu wake kwanza, hulazimisha wengine kuwajibika kwa ajili yake, ama sivyo hununa au huzira na hata kuvunja ukairbu na mtu kwa sababu tu hakusaidiwa jambo ambalo ni wajibu wake. Wale watu 10 nyuma ya watu. kila mmoja ajitafakari anavyowatendea watu wake wa karibu pale wanapotegemea sapoti yake. Tujiulizetunaangukia kwenye kundi gani? Darasa linakutakia tafakuri njema.

Friday, August 11, 2023

Darasa 38: Hakuna asiye na cha kutoa na hakuna asiyehitaji

Darasa linakukumbusha kuwa.......… Usiache kuwa jambo zuri kwa watu wengine hata wakati ule unapopitia magumu yako. Kuna watu wanaishi maisha ya kulalamika kila siku. Wao hivi wao vile. Kuna watu ni wenye kujiona wanastahili kupokea tu na si kutoa kwa sababu hawana pesa, au hawana hiki au kile. Kuna watu wamejipa hatimiliki ya kutendewa mema na si kutenda. Rafiki, hata katikati ya magumu yako nenda ukawe jambo zuri kwa mtu. kuna namna nafsi yako itainuka. Kuna baraka utaichota. Nenda kawe jambo zuri kwa mtu. Kwa maneno au vitendo; kwa maneno na vitendo. Kaweke tabasamu usoni pa mtu. Darasa linakutakia tafakuri njema.



DARASA la Laura Pettie ni makala zinazokujia kila Jumanne na Alhamis kupitia akaunti yetu ya YouTube. Unaweza kusikiliza makala zote kwa  leo kubofya PLAYLIST HII au tembelea akaunti yetu hii ya YouTube

Mawaidha ya ijumaa 11.8.2023 "Mazuri tunayo yakosa kwa kuchelewa kuswali jamaa"

Leo kwenye mawaidha ya ijumaa 11.8.2023 unatazama hotuba kutoka kwa Sheikh Salim Mubaraka Sazi wa masjid Abuu-bakari uliopo Mlandege Manispaa ya Iringa, akitukumbusha kuhusu "mazuri tunayoyakosa kwa kuchelewa kuswali jamaa".

Monday, April 19, 2021

255 Info Package ya Kwanza Radio EP06 Aprili 19, 2021

Karibu kwenye show kabambe yenye muziki na habari mbalimbali za muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania. Mr Presenter anakupitisha kwenye taarifa mbalimbali za kimuziki ikiwemo mgodi wenye habari mbalimbali za muziki na wanamuziki wa Bongo Flava. Leo atasikika mkongwe Adili Chapakazi, wasanii G-Nako, Hamadai, Iddo the Gold na Moni Centrozone Ni kila Jumatatu saa kumi kamili kwa saa za Afrika Mashariki, na marudio ni saa kumi kamili kwa saa za Marekani ya Mashariki. Kwanza Radio itapatikana punde online saa 24 kupitia tovuti yetu www.kwanzaproduction.com Kwa sasa tusikilize kupitia Radio Garden radio.garden/listen/kwanza-radio/ZUtbxgBv OnlineRadio Box onlineradiobox.com/us/kwanza/?cs=us.kwanza TuneIn tunein.com/radio/Kwanza-Radio-s290047/

Sunday, April 18, 2021

AFRO KWANZA ya Kwanza Radio EP06 Aprili 17, 2021

Karibu kwenye show ya muziki wa kiAfrika ikiandaliwa na Mussa Yusuph.Leo utapata habari zaidi juu ya wasanii Oliver Ngoma, Tshala Mauna na Awilo Longomba. Kipindi hiki hukujia kila Jumamosi kuanzia saa kumi kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki, na marudio ni saa kumi jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki. Tutakujia punde kupitia tovuti yetu www.kwanzaproduction.com Kwa sasa unaweza kusikiliza radio kupitia Radio Garden http://radio.garden/listen/kwanza-radio/ZUtbxgBv OnlineRadio Box https://onlineradiobox.com/us/kwanza/?cs=us.kwanza TuneIn https://tunein.com/radio/Kwanza-Radio-s290047/ Kama umekikosa, basi punde baada ya kupindi, bofya https://soundcloud.com/kwanzaproduction/afro-kwanza-ya-kwanza-radio-ep06-aprili-17-2021 https://soundcloud.com/kwanzaproduction/afrokwanza-ep05  

Saturday, April 17, 2021

DONDOO NA REGGAE ya Kwanza Radio. Kazi za Lucky Dube

Jambo ambalo bado nawaza kuhusu Lucky Dube ni uwezo wake wa kuwaza kitu ambacho kipo, na ambacho kingeweza kutendeka kwa namna fulani lakini hakikutendeka hivyo japo kinaleta maana halisi ya fikra ya kutendeka kwake. 
Yaani alikuwa na uwezo mkubwa saana wa KUSADIKI habari ama tukio ama maisha halisi kwa namna ambavyo yanaweza KUSADIKIKA. 
Alieleza, kuuliza ama kufafanua utata ama fumbo ama mwenendo fulani wa maisha kwa namna ya kipekee. 
Tunaweza kuangalia baadhi ya nyimbo kuwaza kwa pamoja kuwa ALIWAZA NINI?? 

Tutakujia punde kupitia tovuti yetu www.kwanzaproduction.com 
Kwa sasa unaweza kusikiliza radio kupitia 
Radio Garden 
OnlineRadio Box 

255 Info Package ya Kwanza Radio EP05 Aprili 12, 2021

Mr Presenter anakupitisha kwenye taarifa mbalimbali za kimuziki ikiwemo mgodi wenye habari mbalimbali za muziki na wanamuziki wa Bongo Flava. Leo atasikika mkongwe Adili Chapakazi, wasanii G-Nako, Hamadai, Iddo the Gold na Moni Centrozone Ni kila Jumatatu saa kumi kamili kwa saa za Afrika Mashariki, na marudio ni saa kumi kamili kwa saa za Marekani ya Mashariki. Kwanza Radio itapatikana punde online saa 24 kupitia tovuti yetu www.kwanzaproduction.com Kwa sasa tusikilize kupitia 
Radio Garden 
 OnlineRadio Box 
TuneIn 

AFRO KWANZA ya Kwanza Radio EP 05 April 10, 2021

Reggae Time ya Kwanza Radio.. Rastafarianism

Amani, Upendo na Heshima kwako msikilizaji wa Kwanza Radio. Karibu katika kipindi hiki cha Reggae Time, kinachokujia kutoka hapa Kilimanjaro Studios. Na leo, tunagusia mambo kadhaa ambayo ni vema kuyajua kuhusu maRasta. Watu wengi wanaposikia neno RASTAFARI, wanaelekeza fikra zao kwa watu wenye rasta ama dreadlocks, kwa uvutaji wa bangi, kwenye muziki wa Reggae na kadhalika. Lakini, kwa hakika uRasta ni falsafa makini ambayo huchukua mwelekeo mkubwa wa kiImani. Japokuwa wapo wengi ambao hufuata ama kujiita maRasta ili kupata mwanya wa kufanya baadhi ya mambo maovu, ukweli unabaki palepale kuwa wapo wafuasi wazuri wa imani ya uRasta, ambao jamii isiyowajua vema, inawachukulia visivyo. Mubelwa Bandio anakusihi uwe naye pamoja mpaka mwisho. Wewe msikilizaji unaweza kushiriki kwa kutuma ujumbe ama maoni yako kwenye mitandao yetu ya kijamii. Tufuatilie kwenye Facebook, Instagram, Twitter na Soundcloud. Tafuta Kwanza Production.

255 Info Package ya Kwanza Radio EP04 Aprili 4, 2021

Karibu kwenye show kabambe yenye muziki na habari mbalimbali za muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania. Mr Presenter anakupitisha kwenye taarifa mbalimbali za kimuziki ikiwemo mgodi wenye habari mbalimbali za muziki na wanamuziki wa Bongo Flava. Leo atasikika mkongwe Adili Chapakazi, wasanii G-Nako, Hamadai, Iddo the Gold na Moni Centrozone Ni kila Jumatatu saa kumi kamili kwa saa za Afrika Mashariki, na marudio ni saa kumi kamili kwa saa za Marekani ya Mashariki. Kwanza Radio inapatikana online saa 24. Tusikilize kupitia tovuti yetu www.kwanzaproduction.com Pia unaweza kusikiliza radio kupitia Radio Garden http://radio.garden/listen/kwanza-radio/ZUtbxgBv OnlineRadio Box https://onlineradiobox.com/us/kwanza/?cs=us.kwanza TuneIn https://tunein.com/radio/Kwanza-Radio-s290047/